“Hata sasa Bwana ametusaidia”
Mshukuruni Bwana,liitieni jina ,Wajulisheni watu matendo yake. Mwimbieni, mwimbieni kwa zaburi, Zitafakarini ajabu zake zote. Zaburi 105:1, 2.
M
atendo ya Mungu kwa watu wake yapasa yatazamwe tena mara kwa mara. Ni mara ngapi Bwana aliweka alama njiani katika kushughulika na Israeli wa kale! Ili wasisahau historia ya wakati uliopita, alimwamuru Musa kuweka matukio haya katika mfumo wa wimbo, ili wazazi wapate kuwafundisha watoto wao. Iliwapasa wakusanye kumbukumbu na kuziweka kwa namna zinavyoweza kuonekana. Jitihada ya ziada ilifanyika ili kuyatunza, ili wakati watoto watakapouliza kuhusu mambo haya, kisa kizima kipate kuelezwa. Kwa namna hiyo, matukio yaliyotokea kwa wakati sahihi na wema bayana na rehema za Mungu katika uangalizi wake na ukombozi wa watu wake vilikuwa katika akili zao. Tunashauriwa hivi; zikumbukeni siku za kwanza, ambazo, mlipokwisha kutiwa nuru, mlistahimili mashindano makubwa ya maumivu” (Waebrania 10:32). Bwana ametenda kama Mungu atendaye maajabu kwa ajili ya watu wake kwenye kizazi hiki… Mara kwa mara tunahitajika kukumbuka wema wa Mungu na kumsifu kwa sababu ya matendo yake ya ajabu.
Hebu tusitupilie mbali ujasiri wetu, bali tuwe na uhakika ulio imara, imara kuliko wakati wowote uliopita. “Hata sasa Bwana ametusaidia,” naye atatusaidia hadi mwisho (1 Samweli 7:12). Hebu tutazame vinara vya kumbukumbu, vinavyotukumbusha kile ambacho Bwana ametenda ili kutufariji na kutuokoa kutoka katika mkono wa mharabu. Hebu na tuweke upya katika kumbukumbu zetu rehema zote ambazo Mungu ametuonesha – machozi ambayo ameyafuta, maumivu ambayo ameyapoza, wasiwasi ambao amuondoa, hofu ambazo amezifutilia mbali, mahitaji ambayo ametupatia, baraka ambazo ametupatia - kwa namna hiyo tunajiimarisha wenyewe kwa ajili ya yote yaliyo mbele yetu kwa njia ya kumbukumbu za safari yetu.
Hatuwezi kuacha kutazama mbele kwenye fadhaa mpya za pambano linalokuja, lakini tunaweza kutazama kile kilichopita pamoja na kile kinachokuja, na kusema, “Hata sasa Bwana ametusaidia.” “Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako” (Kumbukumbu 33:25). Jaribu halitazidi uwezo tutakaokuwa tumepewa kulistahimili. Kwa hiyo, hebu tuchukue kazi yetu kuanzia pale tunapoikuta, tukiamini kwamba chochote kiwezacho kutokea, uwezo kulingana na jaribu utatolewa.
Hebu tusitupilie mbali ujasiri wetu, bali tuwe na uhakika ulio imara, imara kuliko wakati wowote uliopita. “Hata sasa Bwana ametusaidia,” naye atatusaidia hadi mwisho (1 Samweli 7:12). Hebu tutazame vinara vya kumbukumbu, vinavyotukumbusha kile ambacho Bwana ametenda ili kutufariji na kutuokoa kutoka katika mkono wa mharabu. Hebu na tuweke upya katika kumbukumbu zetu rehema zote ambazo Mungu ametuonesha – machozi ambayo ameyafuta, maumivu ambayo ameyapoza, wasiwasi ambao amuondoa, hofu ambazo amezifutilia mbali, mahitaji ambayo ametupatia, baraka ambazo ametupatia - kwa namna hiyo tunajiimarisha wenyewe kwa ajili ya yote yaliyo mbele yetu kwa njia ya kumbukumbu za safari yetu.
Hatuwezi kuacha kutazama mbele kwenye fadhaa mpya za pambano linalokuja, lakini tunaweza kutazama kile kilichopita pamoja na kile kinachokuja, na kusema, “Hata sasa Bwana ametusaidia.” “Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako” (Kumbukumbu 33:25). Jaribu halitazidi uwezo tutakaokuwa tumepewa kulistahimili. Kwa hiyo, hebu tuchukue kazi yetu kuanzia pale tunapoikuta, tukiamini kwamba chochote kiwezacho kutokea, uwezo kulingana na jaribu utatolewa.
No comments:
Post a Comment