Vita Vizuri
Vita Vizuri
Nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, Imani nimeilinda. Baada ya hayo nimewekewa taji ya haki, ambayo Bwana, mhukumu mwenye haki, atanipa siku ile; wala si mimi tu, bali na watu wote pia waliopenda kufunuliwa kwake. 2 Timotheo 4:7,8
K
atika kipindi kirefu cha utumishi, kamwe Paulo hakusita katika utii wake kwa Mwokozi. Popote alipokuwa—iwe ni mbele za Mafarisayo wenye hasira, au mamlaka ya Kirumi; mbele za kundi lenye hasira pale Listra au wenye dhambi walioamini kwenye gereza la shimoni la Makedonia; iwe ni kutoa hoja kwa mabaharia walioshikwa na hofu kwenye mashua iliyovunjika, au kusimama peke yake mbele za Nero kutetea maisha yake—kamwe alikuwa hajawahi kujisikia kuaibika kutetea kile alichokiamini. Kusudi moja kuu la maisha yake ya Kikristo lilikuwa kumtumikia Yeye ambaye jina lake lilimjaza kwa dharau; na kutokana na kusudi hili, hakuna upinzani au mateso ambayo yaliweza kumgeuzia upande mwingine.
Maisha ya Paulo ni mfano wa ukweli aliokuwa akiufundisha na hapa ndipo tunapoona nguvu yake. Moyo wake ulikuwa umejawa na hisia yenye kina ya wajibu wake naye alifanya kazi kwa mawasiliano ya karibu zaidi na Mungu aliye chemchemi ya haki, rehema na kweli….Upendo wa Mwokozi ulikuwa ndiyo dhamira isiyokufa ambayo ilimshikilia kwenye mapambano yake dhidi ya nafsi na kwenye vita vyake dhidi ya uovu kama alivyokuwa kwenye utumishi wa Kristo akisonga mbele dhidi ya kutokuwa rafiki wa dunia na upinzani wa maadui zake.
Kile kanisa linachohitaji katika siku hizi za hatari ni jeshi la watendakazi ambao, kama Paulo, wamejifunza ili wawe wenye manufaa, ambao wana uzoefu wa kina katika mambo ya Mungu na ambao wamejawa na bidii na ari. Watu waliotakaswa, wanaojitoa wanahitajika; watu ambao hawatajitenga na majaribio na wajibu; watu walio jasiri na wakweli; watu ambao mioyoni mwao Kristo ameumbika “tumaini la utukufu,” naye ambaye midomo yake imeguswa kwa moto mtakatifu ata“lihubiri neno.”…
Je, vijana wetu watakubali hii amana takatifu itokayo mikononi mwa baba zetu? Wanajiandaa kujaza nafasi inayoachwa kutokana na kifo cha aliye mwaminifu? Maagizo ya mtume yatatiliwa maanani, mwito kwa ajili ya wajibu utasikiwa, katikati ya uchochezi wa ubinafsi na tamaa zinazowavutia vijana?
Maisha ya Paulo ni mfano wa ukweli aliokuwa akiufundisha na hapa ndipo tunapoona nguvu yake. Moyo wake ulikuwa umejawa na hisia yenye kina ya wajibu wake naye alifanya kazi kwa mawasiliano ya karibu zaidi na Mungu aliye chemchemi ya haki, rehema na kweli….Upendo wa Mwokozi ulikuwa ndiyo dhamira isiyokufa ambayo ilimshikilia kwenye mapambano yake dhidi ya nafsi na kwenye vita vyake dhidi ya uovu kama alivyokuwa kwenye utumishi wa Kristo akisonga mbele dhidi ya kutokuwa rafiki wa dunia na upinzani wa maadui zake.
Kile kanisa linachohitaji katika siku hizi za hatari ni jeshi la watendakazi ambao, kama Paulo, wamejifunza ili wawe wenye manufaa, ambao wana uzoefu wa kina katika mambo ya Mungu na ambao wamejawa na bidii na ari. Watu waliotakaswa, wanaojitoa wanahitajika; watu ambao hawatajitenga na majaribio na wajibu; watu walio jasiri na wakweli; watu ambao mioyoni mwao Kristo ameumbika “tumaini la utukufu,” naye ambaye midomo yake imeguswa kwa moto mtakatifu ata“lihubiri neno.”…
Je, vijana wetu watakubali hii amana takatifu itokayo mikononi mwa baba zetu? Wanajiandaa kujaza nafasi inayoachwa kutokana na kifo cha aliye mwaminifu? Maagizo ya mtume yatatiliwa maanani, mwito kwa ajili ya wajibu utasikiwa, katikati ya uchochezi wa ubinafsi na tamaa zinazowavutia vijana?